NYAMA YA MBUZI KWA MAPISHI TOFAUTI

 NYAMA YA MBUZI KWA MAPISHI TOFAUTI

































Mahitaji

  • Nyama ya mbuzi – kilo 1
  • Vitunguu maji vikubwa - 2.
  • Nyanya za kawaida - 6 (ukipenda unaweza nunua na ya kopo).
  • Kitunguu swaumu - 1
  • Tangawizi
  • Karoti
  • Hoho
  • Kolimaua
  • Njegere
  • Mafuta
  • Chumvi
  • Maji
  • Bizari
  • Maelekezo

    • Katakata nyama, osha kisha weka vitunguu swaumu na tangawizi. Ache nyama pembeni kama nusu saa ili viungo viingie vizuri.
    • Andaa karoti, vitunguu, nyanya, kwa kukata vipande vidogo vidogo.
    • Menya viazi, osha, kata vipande vidogo kisha hifadhi kwenye sufuria ya maji ili visibadilike rangi.
    • Andaa tangaziwi, vitunguu swaumu kwa kukata na kisha kuponda kwenye kinu
    • Bandika mafuta yakichemka tia vitunguu maji vyote vikaange mpaka viwe vinakaribia kubadilika rangi
    • Weka nyama ya mbuzi huku unaendelea kukoroga
    • Weka chumvi, koroga ili ichanganyike vizuri.
    • Weka pilipili hoho, carrots, kolimaua na njegere. Koroga kwa takribani dakika tano.
    • Weka nyanya koroga kiasi na kisha funika na mfuniko.
    • Mchanganyiko ukiiva weka nyanya ya kopo na maji kiasi ili kuivisha nyama.
    • Weka viazi ili vipate kuiva na mchanganyiko wa nyama.
    • Ili kuongeza ladha, weka bizari (au kiungo chochote cha kuongeza ladha ya chakula).
    • Funika nyama yako kwa muda wa dakika ishirini.
    Nyama itakuwa tayari imeiva na unaweza kula na chakula upendacho.Viazi ulaya

Comments